const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); WANAWAKE WATAKIWA KULAZIMISHA KWENDA MAHAKAMANI NDOA ZINAPOVUNJIKA - HABARI MPYA

..

WANAWAKE WATAKIWA KULAZIMISHA KWENDA MAHAKAMANI NDOA ZINAPOVUNJIKA

Post a Comment
WANAWAKE nchini wametakiwa kuhakikisha kuwa wakuwa mashahidi wakati wa kuandikwa waraka wa mirathi ili kuondoa unyanyasaji pindi waume zao wanapo fariki na kunyang’anywa mali huku ambao hawajafunga ndoa wanapo achana wakitakiwa kufika mahakama ya mwanzo kwaaji ya kupata hakizao katika mgawanyo wa mali.

Hayo yanaibuka wakati wanawake wafanyakazi wakitoa elimu kwa wanawake wenzao ambao sio wafanyakazi ili kuzijua haki zao kabla hayajawakuta manyanyaso baada ya kubaki wajane.

Wakiuliza maswali kwa maafisa ustawi wa jamii na wanasheria mjini Njombe wanasema kuwa wakiwa wameolewa katika ndoa ya mitala wanahaki ya kupata mali huku wengine wakiuliza kuhusu wosia unapo andikwa nani anatakiwa kuwepo.

Wakijibu maswali kutoka kwa wakinamama, mwanasheria, taasisi za kisheria na ustawi wa jamii wanasema mke na watoto katika mirathi ni mashahidi wa kwanza.
Afisa ustawi wa jamii mkoa wa Njombe anasema kuwa wameamua kutoa elimu hiyo ili kuwakwamua wanawake na masuala ya unyanyasaji iliwa ni moja ya shughuli za kuadhimisha siku ya wanawake duniani.
VIDEO YA HABARI HAPO JUU HII HAPA CHINI TANZAMA............................



JE UMEPITWA NA HII BOFYA PRAY KUTAZAMA WALICHO WANYA WANANZENGO...............

ꜜꜜꜜ

Related Posts

Post a Comment