const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); ASILIMIA 80 YA FEDHA ZA SERIKALI ZINAINGIZWA KATIKA MFUMO WA MANUNUZI YA UMMA - HABARI MPYA

..

ASILIMIA 80 YA FEDHA ZA SERIKALI ZINAINGIZWA KATIKA MFUMO WA MANUNUZI YA UMMA

Post a Comment
ASILIMIA 80 ya fedha za serikali zinaingia katika manunuzi ya umma ambako zinatekeleza miradi mbalimbali na zingine zikitumika isivyo katika michakato mbalimbali ya kutekeleza miradi ya maendeleo ya umma hapa nchini.
Waandishi wa nyanda za juu kusini, kusini na Mkoa wa Dodoma wanapewa mafunzo ili kwenda kufichua madudu na kuweka wazi mbivu na mbichi ili kuokoa mabilioni ya serikali yanayo wekezwa katika miradi na kutumika isivyo na kusababisha hasara kwa serikali na jamii.
Asilimia hizo zinawekwa bayana kwa wandishi wa habari na kuwa serikali asilimia 20 ambapo Mmlaka ya manunuzi ya umma PPRA inasema kuwa waandishi wakipatiwa elimu juu ya manunuzi ya umma na sheria zake wanaweza kuokoa fedha na kufichua wanao fanya uharibifu.
Waandishi nao wanasema kuwa baada ya mafunzo haya wanatarajia kuandika kwa weledi juu ya manunuzi ya umma.
Kwa mujibu wa sheria za manunuzi waandishi wanatakiwa kuwapo wakati wa ufunguzi wa tenda yoyote na kuwa jamii pia inatakiwa kujua kama kunatenda yoyote ile kwa kutangazwa katika Magazeti yanayo somwa na watu wengi hapa nchini na maeneo mengine.
WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU kUSINI, KUSINI NA DODOMA WAPO MBEYA SIKU TATU ................

Related Posts

Post a Comment