const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); TzTown Tv: Wanging'ombe kujipanga kujenga soko la Nyanya - HABARI MPYA

..

TzTown Tv: Wanging'ombe kujipanga kujenga soko la Nyanya

Post a Comment
KATIKA kuhakikisha kuwa kila halmashauri inakuwa na kitega uchumi Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe inatarajia kuaza ujenzi wa soko la kubwa kwaajili ya biashara ya Nyanya na kuwasaidia wakulima kupata mahara pa kuuzia nyanya.

Halmashauri hiyo imebaini kuwa kuna wakulima wao wengi wanalipa ushuru katika halmashauri Nyingine wakati wao wanauwezo wa kuwa na soko la nyanya na wakapata maendeleo kutokana na pesa zao za Ushuru wa Mazao.

Mradi huo umebuniwa na halmashauri ya wilaya hiyo katika vikao vyake vya halmashauri lakini kinacho wakwamisha mi mtaji wa ujenzi wake Mwenyekiti wa halmashauri Hiyo anasema ujenzi unategemea mapato ya Ndani.

Hata hivyo diwani wa eneo linapotakiwa kujenga soko hilo anakili kuwapo kwa bajeti ndogo ya mapatio ya ndani ya halamashauri kwajili ya ujenzi wa soko hilo.
Kutokana na bajeti Ndogo nini inatarajia kufanya halmashauri kama mpango wa awali kuanzisha soko hilo

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa mkoani Njombe hivi karibuni anazitaka halmashauri kujitafutia vyanzo vya mapato ili kujiinulia kupato na kutoa huduma bora kwa jamii

Related Posts

Post a Comment