const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); Chadema Njombe wasema hawata shirikiana na Mkuu wa Wilaya - HABARI MPYA

..

Chadema Njombe wasema hawata shirikiana na Mkuu wa Wilaya

Post a Comment
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilaya ya Njombe kimesema hakitafanya kazi na mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafiri kama hataomba radhi ndani ya siku saba kwa kumuweka ndani mwenyekiti wa mtaa wa Bunguruni Emmanuel Ngelime tukio ambalo lilitokea Mwishoni mwa mwezi jana mwaka huu.
Chama kimesema kuwa kitendo hicho hakikubaliki na uongozi wa wilaya hautakubaliana na tukio hilo alilofanyiwa mwenyekiti mwenyekiti wao.

Viongozi wa wilaya, madiwani na wenyeviti wa mitaa kupitia Chadema wanaketi kikao cha siku tatu cha kutafakari juu ya jambo alilolifanya mkuu wa wilaya ya Njombe la kumuweka ndani kwa masaa 48 mwenyekiti wa mtaa.
Madiwani kupitia chama hicho wanasema kuwa hawapo tayari kushirikiana na mkuu hiyo wa wilaya kwa wakipinga kile alicho kifanya kwa mwenyekiti huo.

Mwenyekiti wa chama hicho wilya ya Njombe Abuu Mtamike ambaye pia ni diwani wa kata ya Mjimwema anasema kuwa wanatoa tamko la kuto shirikiana naye katika shughuli yoyote ya kimaendeleo na kuwa wanamtaka aombe msamaha ndani ya siku saba.

Mkuu wa wilaya ya Njombe mwishoni mwa mwezi jana kwa mujibu wake alimuweka ndani mwenyekiti huyo kwa madai ya kumtolea maneno machafu mkuu huyo wa wilaya baada ya kumtaka aachie ngazi ya uongozi baada ya kuhukumiwa kifungo cha nje kwa mwaka mmoja na mahakama.
TAZAMA VEDEO MKUU WA WILAYA AKATATIWA KUFANYA KAZI NA CHADEMA.................

Related Posts

Post a Comment