const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); Mambo Hadhari Kashfa Nzito,Mke Wa Deo Filikunjombe Adaiwa Kutoka Na Waziri - HABARI MPYA

..

Mambo Hadhari Kashfa Nzito,Mke Wa Deo Filikunjombe Adaiwa Kutoka Na Waziri


Mambo ni moto! Ubuyu ulionyooka uliolifikia gazeti hili unadai kuwa, waziri mmoja mchapakazi (jina tunalihifadhi kwa sasa), anadaiwa kurithi mikoba ya aliyekuwa Mbunge wa Ludewa mkoani Njombe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), marehemu Deo Haule Filikunjombe kwa ‘kujiweka’ kwa mkewe, Sarah Habiba, Ijumaa lina habari kamili.Awali, vyanzo vilivyo karibu na Sarah, vilishusha madai kuwa, waziri huyo kijana, amekuwa akitinga nyumbani kwa marehemu anapoishi Sarah na watoto wake watatu wa kiume, Mtoni-Kijichi jijini Dar.

“Yaani tunashangazwa sana na ujio wa huyu waziri. Unajua bora kama ingekuwa ni mtu wa mbali, lakini huyu alikuwa karibu sana na marehemu Deo na anamfahamu vizuri, iweje leo aje amrithi rafiki yake?
“Si mara moja au mara mbili, tunamuona mara kwa mara anakuja hapa nyumbani. Akija anakaa weee…baadaye ndo’ anaondoka. “Unajua hii haileti picha nzuri. Bora hata angekuwa mtu wa mbali, lakini si huyu ambaye alikuwa akimfahamu vizuri marehemu. Hii inaleta picha kwamba huenda alikuwa akimtamani mke wa mwenzake hata kabla Deo hajafariki dunia,” Chanzo kilishusha madai hayo mazito.

MADAI ZAIDI

Chanzo hicho kilizidi kushusha madai kwamba, waziri huyo ndiye ambaye anampa kampani Sarah hata kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia hivyo kuashiria kuwa wawili hao ni ‘damdam’.
“Waziri ana mawe, nasikia ndiye anayesimamia mpango mzima hadi mambo ya shule ya watoto pamoja na vurugu za Sarah, mheshimiwa anakata mkwanja,” kilidai chanzo hicho.

MKE WA DEO AANIKA UKWELI
Baada ya kupata madai hayo, Ijumaa lilimtafuta mke wa Deo na kumwekea mezani madai hayo yote ambapo aliyakanusha vilivyo na kusema anayashangaa yametokea wapi.

“Siyo kweli. Nasema siyo kweli, hivyo vitu ninashindwa kuelewa hata vinatokea wapi? Wanaleta hayo maneno bila kuwa hata na ushahidi wala ukweli wowote.

“Sasa hebu angalia wanasema kuhusu watoto wewe mwenyewe (anataja jina la mwandishi) unajua, watoto ninawasomesha mwenyewe. Namshukuru Mungu najimudu kuwasomesha wanangu na kufuatilia maendeleo yao kimasomo,” alisema Sarah.

Related Posts

Post a Comment