const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); TzTown Tv: Waziri Mkuu akiwa Njombe amwagiza mkuu wa mkoa kuchunguza ankra za maji - HABARI MPYA

..

TzTown Tv: Waziri Mkuu akiwa Njombe amwagiza mkuu wa mkoa kuchunguza ankra za maji







WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya muungano Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amemuagiza mkuu wa Mkoa wa Njombe Kuunda tume ya siku moja kuchunguza suala la bili za maji na mfumo uliotumika kupandisha bili za maji mjini hapo na baada ya hapo serikali itatoa maamuzi.

Agizo hilo linatolewa katika mkutano wa hadhara ambapo mbunge wa Njombe Mjini Mhe. Edward Mwalongo ambaye ametoa malalamiko ya wananchi mbele ya waziri Mkuu ambapo serikali inasema kuwa imeandaa fedha kwaajili ya kumamilisha miradi mbalimbali.

Ni mabango ambayo yanaambatana na kerere za shangwe ambazo zinampokea huku nyimbo nazozikichagiza.

Mbunge anasimama mbele ya kipaza na kuwasemea wananchi ambapo miradi ya maji ikitawala maombi yake na kusema kuwa kuna miradi mikubwa inasuasua.

Waziri Mkuu anaanza na bili za maji kwa kumuita mkurugenzi wa Maji halmashauri ya Mji Njombe Daudi Majani kuelezwa wananchi ambapo anabaini madudu.

Hata hivyo waziri mkuu anatoa agizo kwa mkuu wa mkoa wa Njombe kuhusu masuara kupanda kwa bei ya maji na matumizi ya fedha za maji zinazo kusanywa.

Masuala mengine yaliyo ibuka katika mkutano wake ni pamoja na ardhi barabara na huduma za Afya ambapo serikali inaekezwa kuwa imetwenga Bilioni 200 kwaajili ya dawa pekee na zimekabishiwa kwa bohari ya dawa MSD na kuwa malengo ya serikali ni kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana kula pahala palipo na wananchi.

Waziri mkuu kabla ya kukutana na wananchi wa mji wa Njombe anatembelea stendi ya mabasi ya mkoani Njombe inayo jengwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi bilini 9 za kitanzania lakini kauli ya serikali akiwa hapa inatolewa na mkuu wa mkoa kuachiwa jukumu huku ziara yake ikihitimishwa mkoani Njombe anakutana na watumishi wa serikali.

TAZAMA VIDEO HAPA WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA WAKAZI WA NJOMBE NI KUHUSU MAJI, AFYA 



Related Posts

Post a Comment