const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); AGIZO LA RAIS MAGUFULI LASABABISHA MADIWANI WA CHADEMA KUZICHAPA KIKAONI - HABARI MPYA

..

AGIZO LA RAIS MAGUFULI LASABABISHA MADIWANI WA CHADEMA KUZICHAPA KIKAONI

Agizo alilolitoa Rais Dkt John Pombe Magufuli la kutaka Baraza la Madiwani la Jiji la Dar es Salaam likutane kuamua matumizi ya fedha zilizolipwa kununua hisa za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), limezua tafrani baada ya makada wawili wa CHADEMA kuzichapa kavukavu kikaoni.

Rais Dkt Magufuli alitaka baraza hilo likutane kuajadili matumizi ya TZS bilioni 5.8 zilizolipwa na kampuni ya UDART inayoratibu mabasi yanendayo haraka kukamilisha ununuzi wa hisa za UDA.

Madiwani hao walipokutana jana kwenye kikao kuliibuka vurugu hizo baada ya kupisha kimtazamo juu ya matumizi ya fedha hizo.

Mvutano huo ulikuwa baina ya pande mbili ambapo, upande mmoja walitaka uamuzi wa kutumia fedha hizo usipitishwe kwa madai kuwa mchakato wa uuzaji wa hisa hizo kwa UDART haukufuata sheria wala taratibu, wakati upande mwingine ukitaka uamuzi upitishwe.

Wajumbe wa Chadema walioshikana mashati walipokuwa katika kikao cha pembeni cha madiwani wa chama hicho baada ya mkutano wa Baraza la Madiwani kumalizika ni, Boniface Jacob, Meya wa Ubungo na Patrick Assenga ambaye ni Diwani, Tabata.

Viongozi hao walifikia hatua hiyo baada ya kile walichokuwa wakibishania kuwa ni kutosimamia msimamo wa chama ambao wanataka fedha hizo zisitumike kwani wanaamini sheria na taratibu za uuzwaji wa hisa hazikufuatwa.

Related Posts

Post a Comment