Utafiti uliofanywa na Wanasayansi kutoka National Research Council umegundua kuwa ulaji wa chipsi au viazi vilivyokaangwa mara mbili au zaidi kwa wiki husababisha vifo vya mapema kwa vijana kwa zaidi ya 70%.

Katika utafiti huu watu 4,440 walihusishwa na walikula chipsi mara tatu kwa wiki kwa muda wa miaka minane ambapo zaidi ya watu 236 walifariki kutokana na ugonjwa wa cardiovascular kuliko magonjwa mengine.
Aidha, wa mujibu wa utafiti huo, imebainika kwamba ukiacha matatizo kama unene kupita kiasi na ugonjwa wa kisukari,ulaji wa chipsi umetajwa kuwa hatari zaidi kwa kusababisha magonjwa yanayopelekea vifo vya haraka.
Post a Comment
Post a Comment