const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); Tumia kitunguu maji kutibu sikio - HABARI MPYA

..

Tumia kitunguu maji kutibu sikio


Sikio pua na koo ni viungo vinavyohusiana kwa ukaribu sana kiasi kwamba linapotokea tatizo katika kiungo kiojawapo, tatizo hilo pia huweza kujitokeza pia katika kiungo kingine.

Mfano inapotokea pua zimeziba, basi masikio pia yanaziba au sikio linapouma pia pua huweza kutoa kamasi hali kadhalika na koo linapouma wakati wa kumeza chakula sikio pia linauma.

Miongoni mwa sababu zinazoweza kusababisha maumivu ya sikio pamoja na uwepo wa jipu au upele ndani ya njia, kelele za nguvu, kupenga kamasi kwa nguvu, kukaukiana kwa nta ndani ya sikio.

Mara nyingi maumivu mengi ya sikio huwa yanakubali matibabu kwa urahisi.

Zipo tiba mbalimbali za sikio linapokuwa na maumivu, lakini kwa leo nitakufahamisha hii ya kutumia kitunguu maji ambacho ni rahisi hata kukipata katika mazingira yetu ya kila siku.

Unachopaswa kufanya ili kukamirisha tiba hii ni kuchukua kitunguu maji kisha tengeneza juisi yake na baadaye utatumia matone matatu hadi matano katika sikio.
Fanya hivyo, mara tatu kwa siku kwa muda wa siku tano, Tiba hii ni mahususi kwa sikio linalouma au ambalo limeziba kutokana na kujaa nta.

Tiba za sikio zipo nyingi sana, lakini leo nimekufahamisha hii ya kitunguu maji, hivyo ni kusihi uendelee kuwa karibu na tovuti hii kila siku ili ufahamu tiba nyingi zaidi kutoka kwetu.

Related Posts

Post a Comment