const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); VIWANDA HAVITA SIMAMA KWAAJILI YA MIGOGORO - HABARI MPYA

..

VIWANDA HAVITA SIMAMA KWAAJILI YA MIGOGORO

Post a Comment


Waziri mkuu Kassim Majaliwa akipokea maelezo kutoka kwa Meneja wa kiwanda cha Chai Lupembe alipotembelea kiwandani hapo.

SERIKALI imesema kuwa haita kubali kuendelea kusimamisha viwanda kwa sababu wa migogoro baina ya viwanda hivyo na vyama vya ushirika kwa maslahi ya watu wachache na kuwa viwanda vitaendelea kufanyakazi wakati matatizo yakishighulikiwa na serikali.

Kauli hiyo inatolewa na waziri Mkuu wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa ambayo ameitoa alipo tembelea kwenye kiwanda cha Chai ya Lupembe mkoani Njombe ambacho kilisimama kwa muda na kusababisha miundombinu yake na mali zake kudaiwa kuhujumiwa.

Waziri mkuu anaingia mkoani Njombe kwa mara ya pili ndani ya mwenzi huu na kutembelea kiwanda cha Chai Lupembe na kusema kuwa serikali haita kubari kiwanda kusimama kufanya kazi bali itahakikisha migororo inayosumua viwanda hapa nchini.

Waziri Majaliwa anasema kuwa serikali itahakikisha inafufua viwanda vilivyo fungwa kwa kushindwa kuendesha na kuhakikisha kuwa vipya navyo vinafunguliwa ili watanzania kupata ajira humo.

Amesema kuwa watanzania waendelee kuzalisha malighafi na zitafanyiwa uchakataji hapahapa nchini na kuhakikisha kuwa nchi za nje zinachukua mali ambazo tayari zimesha ongezewa thamani.

Waziri mkuu baada ya kutembela kiwanda hicho anakutanana wananchi wa kijiji cha Igombola  ambapo anasema kuwa wanakulima waendelee kulima chai na kupeleka kiwandani hapo kwa kuwa hakita simama.

Pamoja na mambo mengine waziri majaliwa anasema kuwa matatizo ya maji serikali itashughulikia mgogoro baina ya bodi ya maji inayo maliza mdawake na iliyo po sasa kwa kumtua mkuu wa wilaya hiyo ya Njombe kufika kijijini hapo kutatua tatizo hilo.

Mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafili anasema kuwa serikali itahakikisha kuwa wananchi wanapata maji bila kuwapo kwa vikwazi na Februari 2 mwaka huu kuingia katika kijiji hicho kukutana na viongozi ili kutoa suruhu.

 Kuhusu umeme Shirika la Umeme linasema kuwa tayari kijiji hicho kimetengewa Kipooza umeme na ngunzo zinaanza kusimikwa wiki ijayo na kuanza kusambaza umeme majumani.


Related Posts

Post a Comment