Sehemu ya jengo la Kampuni ya Mkombozi Mwanza yaungua moto.


Sehemu ya ghorofa ya tano ya jengo la Kampuni ya Mkombozi Fishing and Marine Transoprt lililopo Kirumba Mwaloni katika Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza imeungua kwa moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika. Jengo hilo linalomilikiwa na mfanyabiashara wa jijini Mwanza Kitana chacha ujenzi wake bado haujakamilika.

 ITV ilifika katika eneo la tukio hilo na kukuta wananchi wakishirikiana na askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mwanza kuzima moto huo uliokuwa umeteketeza mbao zinazotumika kwa ujenzi wa ghorofa hilo, huku Afisa mafunzo na habari wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Mwanza Mkaguzi Msaidizi Gadaffi Masoud akifafanua kuhusu tukio hilo.

Tukio hilo la moto limekuja ikiwa ni wiki tatu baada ya moto mkubwa kuteketeza sehemu ya nyuma ya nyumba ya kulala wageni ya Shinyanga iliyopo mtaa wa Lumumba jijini Mwanza na kusababisha kifo cha mmiliki wa jengo hilo Maduhu Masunga maarufu kama mzee Shinyanga pamoja na kuteketeza silaha mbili,kiasi kikubwa cha fedha na mali mbalimbali ambazo thamani yake haikuweza kufahamika mara moja.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!


Related Posts

There is no other posts in this category.

Post a Comment