TIMU YA WATOTO WENYE ULEMAVU NJOMBE KUSHIRIC OLYMPIC

Post a Comment
Mkoa wa Njombe umeanza kuandaa timu ya watoto wenye Ulemavu wa akili na wenye usonji itayo uwakilisha mkoa huo katika mashindano ya kitaifa yanayotarajiwa kufanyika Zanzibar Mwezi Decemba mwaka huu .
Katika kuhakikisha kikosi kitakachopatikana kinauwakilisha mkoa vyema na kurejea nyumbani na medali za kutosha ,tayari kumeanza kufanyika mchakato wa kusaka vipaji vya kundi hilo maalumu la watoto wenye ulemavu kuanzia ngazi ya halmashauri ambako mchujo mkali utafanyika ili kupata timu yenye wachezaji 15 ambao wata ambatana na watu 3 wa benchi la ufundi kwenda Zanzibar.

Akizungumzia maandalizi hayo mratibu wa Special Olimpics Mkoa wa Njombe Happy Mpete anasema pamoja na mkoa kujikita katika kuandaa timu yenye wachezaji 15 itakaoshiriki mashindano ya  Special Olimpics mwezi dec Kisiwani Zanzibar kwa watoto wenye umri wa miaka 2 hadi 7 , pia mkoa umeanza kuandaa timu nyingine ya watoto walemavu wenye kuanzia miaka 8 na kuendelea.
Amesema lengo la serikali na mashirika mengine ya haki za binadamu kuanzisha michezo ya watu wenye ulemavu hususani viziwi, mabubu ,vichwa vikubwa na michezo mingine ni kutokomoza imani mbaya dhidi ya watu wenye mahitaji maalumu .

Happy Mdende  na Maltina Ngatunga ni miongoni mwazazi ambao wameguswa na kushawishika kupeleka watoto wao kujiunga na mazoezi ya kusaka kikosi cha watoto walemavu wa akili na wenye usonji kitakachouwakilisha mkoa katika mashindano hayo Zanzibar na kueleza jinsi mazoezi hayo yanavyohimalisha viungo vya watoto wao.


Michezo itakayoshindaniwa katika mashindano hayo ni pamoja na Riadha , Kuruka Kamba, Mpira wa pete na Mpira wa miguu ambapo hadi sasa watoto 30 wamesajiliwa na kushuhudia wakianza mazoezi kwa furaha zote

Related Posts

There is no other posts in this category.

Post a Comment