TABIA 4 Zinazoharibu Kinga Zako za Mwili Bila Kujijua..!!!

Kinga ya mwili ni ile hali ya mwili kuwa na uwezo wa kujikinga wenyewe dhidi ya maradhi mbalimbali. 
Mtu anapokuwa na kinga imara za mwili, huepuka kuugua mara kwa mara na kwa kifupi unaweza kusema kwamba kinga ya mwili ndiyo kila kitu katika afya ya binadamu. 


Kuumwa mara kwa mara ni dalili tosha kuwa kinga yako ya mwili imeshuka na hivyo unahitaji kuchukua hatua za kuziimarisha.

Kwa kawaida Mungu alituumba miili yetu ikiwa na uwezo wa kujikinga na magonjwa yote, laikini mwili utaweza kufanya hivyo endapo tu utapatiwa vyakula vinavyohitaji ili kuimarisha kinga zake.

Leo tuangalia aina ya vyakula vya kuepuka ili kuzifanya kinga za mwili kufanya kazi zake vizuri.

1. Mhusika anapaswa kuepuka vyakula vyenye sukari nyingi

Sukari siyo nzuri kwa afya yetu hasa inapotumiwa kupita kiwango. Kiwango cha kawaida cha sukari kinachoruhusiwa kutumiwa ni kijiko kimoja kidogo (teaspoon), kinapozidi hapo huwa kinachangia kudhoofisha mfumo wa kinga ya mwili. Inaelezwa kuwa chupa moja ya soda ina karibu vijiko 6 vya sukari. Hivyo kama wewe ni mnywaji mkubwa wa soda na vinywaji vingine vya aina hiyo, utaona ni kiasi gani unachangia kuharibu kinga zako za mwili.

2. Epuka unywaji wa vileo

Unywaji wa pombe kupita kiasi ni sumu ndani ya miili yetu. hivyo si nzuri pia kwani huweza kuchangia kudhoofisha kinga za mwili.

3. Epuka matumizi ya vyakula vya kukaanga

Vyakula vya kukaanga kama vile chips na vinginevyo, pamoja na vyakula vya kuoka huwa na mafuta mabaya ambayo huwa na tabia ya kutengeneza magonjwa mwilini (fee radicals) ambayo huathiri mfumo wa kinga ya mwili pamoja na chembechembe za nasaba (DNA). Vyakula hivi vinapaswa kuliwa kwa nadra sana au kuepukwa kabisa ikiwezekana.

4. Epuka vyakula vya viwandani (vyakula vya makopo)

Epuka ulaji wa vyakula vya kwenye makopo na badala yake pendelea kula vyakula halisi‘fresh’ na vya asili. Ulaji wa vyakula vya asili, hasa vyakula vitokanavyo na nafaka zisizokobolewa, huwa na idadi kubwa ya vitamini, madini na kamba-lishe ambazo ni muhimu sana katika kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili.

Related Posts

Post a Comment