KOMPUTA YA KIKOSI CHA ULINZI CHA RAIS DONALD TRUMP YAIBIWA

Komputa mpakato ya kikosi cha ulinzi cha rais wa Marekani iliyokuwa na mipango ya jengo la Trump Tower pamoja na taarifa kadhaa nyeti imeibiwa kutoka kwenye gari la askari Jijini New York.
Komputa hiyo imewekewa mfumo wa kudhibiti taarifa, na haina taarifa za siri mno ambazo hazipaswi kuangukiwa mikononi mwa raia wa kawaida.

Komputa hiyo pia inataarifa kuhusiana na uchunguzi wa aliyekuwa mgombea urais wa chama cha Democratic, Bi. Hillary Clinton kuhusiana na kutumia barua pepe yake ya binafsi akiwa Waziri wa Mambo ya Nje.

Related Posts

Post a Comment