Ongezeko la Makosa Makubwa 4208 laripotiwa Pwani

MKOA wa Pwani,umekuwa na ongezeko la makosa makubwa 4,208 yaliyoripotiwa katika mwaka 2016 ambapo makosa ya yaliyochukua nafasi kubwa ni unyang’anyi wa kutumia nguvu,kupatikana silaha na mauaji.

Ongezeko hilo ni la makosa 419 ukilinganisha na makosa yaliyoripotiwa mwaka 2015 yaliyokuwa 3,784 .
Aidha makosa madogo 16,332 yaliripotiwa katika kipindi hicho cha mwaka 2016 ambapo kuna ongezeko la makosa 2,396 ikilinganishwa na mwaka 2015 uliokuwa na makosa 13,936.

Akitoa taarifa ya mwaka uliopita kwa waandishi wa habari,ofisini kwake,kamanda wa polisi mkoani Pwani Boniventure Mushongi ,alisema ,hali hiyo inawapa nguvu ya kuongeza kasi ya kupambana/kudhibiti njia za panya na njama wanazotumia wahalifu.
Hata hivyo alieleza,katika kipindi cha Jan hadi desemba 2016 ,kumekuwepo na baadhi ya matukio yaliyovuta hisia za watu ikiwemo tukio kupatikana kwa miili ya watu saba kwa nyakati tofauti wilayani Bagamoyo.

Related Posts

Post a Comment